Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, August 15, 2012

UJENZI WA BARABARA ZA MABASI YAENDAYO KASI KUPUNGUZA FOLENI ZA JIJI LA DAR?




Mafundi wa ujenzi wa Barabara wakiendelea na kazi ya uchimbaji eneo la katikati ya barabara za jijini Dar es Salaam, ili kujenga Njia ya Mabasi yaendayo kasi, Hapa ikiwa ni eneo la Mkwajuni Kionondoni, ambapo mawazo ya walio wengi ni kuwa baada ya kukamilika kwa mradi huo wa ujenzi wa njia hizo na kuanza kazi kwa mabasi yaendato kasi basi huenda foleni zikawa ndiyo kikomo kama si kupungua. Je nini mawazo yako Mdau juu ya hili mradi hu utakapokamilika Foleni zitapungua ama zitaongezeka?
 Eneo la Bonde la Mkwajuni Kinondoni, ambalo tayari eneo hili la katikati ya barabara lilikuwa limeachwa 'jembamba' sasa wataalam wanatarajia kutushangaza kwa lipi katika eneo hili, ili kupitisha njia hii ya mabasi yaendayo kasi?
 Hapa ni eneo la Bonde la Kawe, Barabara ya Bagamoyo, mafundi wakiendelea na zoezi la kupachika daraja katika eneo hili la barabara hiyo mpya, je kukamilika kwa barabara hii, kutasaidia kupunguza foleni ama kutaongeza foleni kwa kufanya hata wale wenye majumba yao ya kifahari ambao walijenga na kuamua kuhamia mjini na kuyaacha majumba yao na kupangisha ili kukwepa foleni na wao pia wote si watareja na hivyo kuongeza tena msongamano?
 Hapa ni eneo la Lugalo, ukitokea Mwenge, mafundi wakiwa katika harakati za kujenga daraja jipya na kubomoa lile la zamani.
 Hapa ni eneo la Kimara Barabara ya Morogoro, mafundi wakiendelea na zoezi la ujenzi wa Njia ya Mabasi yaendayo kasi.
  Hii ni sehemu tu ya foleni za asubuhi ya jijini Dar es Salaam, hapa ni Barabara ya Ali Hassan Mwinyi, eneo la Oysterbay Polisi kabla ya taa za kuongozea magari za Namanga, leo asubuhi.
Je ipo siku Jiji hili la Dar es Salaam, litakuja kuwa kama hivi barabara nyeupeeeee, baada ya kukamilika mradi huo ama itakuwa ni ndoto?? zaidi tembelea  http://sufianimafoto.blogspot.com/

No comments :

Post a Comment