Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, August 16, 2012

SKYLIGHT BAND YAINGIA KWA KISHINDO 'Joniko Flower' ndani




Mwimbaji wa Bendi Mpya ya Skylight, Sonny Masamba (wa pili kulia), akiwaongoza wenzake kuimba wakati wa kuitambulisha bendi hiyo katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam Agosti 15.2012. Bendi hiyo inayomilikiwa na kampuni ya Skylight Entertainment itakuwa ikiporomosha muziki wake katika mahadhi ya Afropop. Kulia ni Meneja wa Bendi, Aneth Kushaba. 
*******************
Ndugu Wanahabari, tunapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru kwa kuchukua muda wenu katika ratiba zenu ngumu za majukumu yenu kuja kusikiliza yale tuliyowaita kuwaeleza.

Kwa kupitia nyie ndugu zetu,tunaamini ujumbe wetu wa habari njema kwa wapenzi wa burudani nchini zitawafikia kwa haraka na urahisi.

Tunaomba rasmi ushirikiano  wenu katika jambo hili la juhudi zetu za kuleta mapinduzi ya kiburudani katika soko la Muziki wa Bendi Tanzania.

Tunafurahi kuwatangazia Umma wa watanzania wapenda burudani,hasa musiki wa bendi,kuwa SKYLIGHT ENTERTAINMENT COMPANY inawaletea bendi mpya ya mahadhi ya AFROPOP kwenye soko la burudani Tanzania.

Bendi yetu mpya ya Skylight imesheheni wanamziki bora na wenye vipaji vya juu na uzoefu mkubwa katika muziki wa hapa Tanzania na mataifa mbalimbali.Leo tumewaita ili tutambulishe rasmi bendi yetu kwenu na kuwajulisha kuhusu burudani kabambe itakayoletwa kwenu na squad hii kali.

Kuwatambulisha kwenu team nzima ya Skylight ni kama ifuatavyo: Kiongozi wa bendi (Band Manager ) ni Anneth Kushaba, Waimbaji: Anneth Kusheba(AK47), Joniko Flower, Sam Machozi, Sonny Masamba na Marry Lucas.
You might also like:

EAC wasema harufu ya pesa zao inanukia.

No comments :

Post a Comment