Mwanamitindo Remtula akiwa katika pozi tofauti.
Na Andrew Chale
Mwanamitindo
 maarufu hapa nchini Ally Rehmtullah ameandaa onyesho kubwa na la 
kipekee la mitindo hapa nchini litakalofanyika tarehe 8 Mwezi ujao 
katika jiji la Dar es Salaam na litarushwa moja kwa moja katika mtandao 
wa www.ar.co.tz bure kabisa ambapo atazindua rasmi kazi zake mpya za mitindo ya mavazi mbalimbali kwa wanaume na wanawake.
Akizungumza
 na vyombo mbalimbali vya habari hivi karibuni, Rehmtullah alisema 
dhumuni la kuandaa onyesho hilo la kipekee ni kuweza kuonyesha aina mpya
 ya mitindo ya mavazi aliyobuni hivi karibuni na harakati zake za kuinua
 kiwango cha kazi za mitindo ndani ya nchi.
“Nimepania
 kupanua wigo wa taaluma ya mitindo na mavazi hapa nchini ili kazi za 
wanamtindo na wabunifu wa mavazi hapa nchini ziweze kupenya kwenye soko 
la ndani na la Afrika mashariki na ya kati wakati tayari kuna soko la 
pamoja katika jumuiya ya Afrika mashariki,’ alisema.
Rehmtullah
 alisema kwamba onyesho hilo litakuwa la kipekee kwa sababu mavazi na 
onyesho litapambwa na rangi nyeupe,ubunifu wa hali ya juu pamoja na 
muonekano mpya wa mavazi yaliyofanyiwa utafiti mkubwa ili kuweza 
kuendana na utamaduni wa mwafrika.
Alisema
 onyesho hilo ambalo litafanyika katika hoteli ya Serena litapambwa na 
wasanii mbalimbali wa muziki na wacheza shoo toka sehemu mbalimbali hapa
 nchini.
Rehmtullah
 alisema onyesho hilo itakuwa ni nafasi ya kipekee kwa yeye binafsi 
kuonyesha muonekano mpya wa tasnia ya mitindo hapa nchini na nje ya 
nchini ili kuonyesha ni kwa jinsi ngani wanamitindo wa kitanzania 
wanavyoweza kuonyesha kazi zao.
Alisema
 kuwa tasnia ya mitindo kwa ujumla ina nafasi ya kipekee kwa wanamtindo 
chipukizi hapa nchini kujitokeza na kuonyesha kazi zao kwa watu 
mbalimbali hasa washika dau katika sekta hiyo.
‘kazi
 za mitindo na mavazi ndio mkombozi wa kweli katika kupunguza tatizo la 
ajira nchini Tanzania kwa sababu ni sekta inayokua kwa kasi kubwa na 
inatoa ajira kwa vijana wengi wa kike na kiume,’aliongeza
Onyesho
 hilo linategemewa kuhudhuriwa na watu zaidi ya 400 wakiwemo viongozi 
mbalimbali kama mawaziri, wabunge, wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa 
mashirika mbalimbali.
Onyesho hilo litakuwa ni la mialiko maalum na limepewa jina la Ally Rehmtullah 2013 collection.
Wadhamini
 wa onyesho hilo ni Mercedez Benz, Belvedere Vodka, DULUX, RAHA, HUGO 
DOMINGO,THE Tanzanite Experience, Shiva Images, Farm Plant, Creative 
Infinities, Out Door, Stanbic Bank, Phoenicia Properties, Dar es Salaam 
Serena Hotel, Missie Popular Blog, Mo Blog, Quality Furniture na Mx 
Carte




No comments :
Post a Comment