Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, July 4, 2012

KAMPUNI ya simu za mkononi Zanzíbar ZANTEL kudhamini tuzo za wanamuziki bora Zanzibar





Na Ali Issa   Maelezo Zanzíbar    
                                                        
KAMPUNI ya simu za mkononi Zanzíbar ZANTEL imeahidi udhamini wa Shl. milioni 32 pesa taslimu kwa Kampuni ya Zanzibar Medium Corporación  kwa ajili ya tunzo ya wana muziki bora wa Zanzíbar mwaka 2012.
Udhamini huo umetangazwa leo na Mkurugenzi wa Biashara Zantel upande wa Zanzibar Mohammed Mussa wakati akizungumza na wandishi wa habarí katika ukumbi wa Idara ya Habarí Maelezo mjini Zanzíbar.
Amesema pesa hizo zimetolewa kwa ajili ya kudhamini tunzo hiyo ikiwa ni njia moja wapo ya kuthamini na kuheshimu mchango ambao wanamuziki wa Zanzíbar wamekuwa wakiutoa ikiwa ni pamoja na kuielimisha na kuiburudisha jamii. 
Ameongeza kuwa Kampuni ya kizalendo ya Zantel imekuwa ikitoa huduma zake na kujenga mapenzi ya dhati kwa jamii ikiwemo kujenga visima vya maji sita ili kuhakikisha faida inayopatikana inaifaidisha jamii kwa ujumla
Mkurugenzi huyo alisema pesa hizo zitatolewa kwa kuzingatia misingi imara na kuepuka upendeleo na kwamba Zanzitel itaendelea kuwa karibú na jamii kwa kutoa ushirikiano pale ambapo itahitajika.
Kwa upande wake Meneja Masoko kutoka Kampuni ya Zanzibar Medium Corporación ambao ndio waandaaji wa tunzo hiyo Said Khamis aliishukuru kampuni ya Zantel kwa kudhamini tunzo hizo na kuiomba indelee kuwa karibú na jamii pale ambapo watahitajika kutoa msaada wao.
Aidha amefahamisha kuwa tunzo hizo ambazo zitatolewa zitakuwa zimegawika katika makundi 1ya aina mbali mbali za wasanii ikiwemo makundi ya muziki wa kizazi kipya (Zenji Fleva) na Taarab asilia.
Tamasha hilo la saba litafanyika Bwawani siku ya Ijumaa,Juni 6 mwaka huu ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamo wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa  Tanzania Dk.Mohammed Gharib Bilali

No comments :

Post a Comment