
Tango ameibuka kinara kwa kupiga mikwaju pointi 38 katika mtindo wa Stable Ford katika mashimo kumi na nane.
Katika kundi A nafasi imekwanda kwa Idan Mziku mikwaju pointi 33, akifuatiwa na Laulence Pangani kutoka katika kundi B aliyepiga mikwaju pointi 37 huku Kei Mwakawago mikwaju point 36 kutoka kundi C akifuatiwa na mwadada Maniwe Pangani mikwaju pointi 37.
Mashindano hayo yenye lengo la kukuza nba kuendeleza mchezo huo hapa nchini yalikuwa na jumla ya washiriki 27 waliogawanyika katika makundi mbalimbali.
Wakatihuohuo, mashindano ya wazi ya Safari maarufu kama Safari Open yataanza kuvurumishwa jumamosi ya wiki viwanjani hapo.
Mashindano hayo ya siku mbili yatachezwa katika mtindo wa Stroken Play katika viwanja 18 na yatashirikisha wachezaji wote wanaoshiriki mchezo huo hapa nchini.
Hadi sasa washiriki zaidi ya 100 wamejiandikisha kushiriki mashindano hayo akiwemo Hamis Ally Idan Mziku na Jane Molell.
No comments :
Post a Comment