
Zimbabwe iliizaba Mauritius 3-0 katika mchezo wa ufunguzi lakini walienda sanjari ya 2-2 na Lesotho.
Lesotho waliwakabili Mauritius huko Harare huku wakitakiwa kushinda 4 bila ili watinge hatua ya Robo Fainali lakini waliishia kuwazima Mauritius bao 1 kwa bila.
Mashabiki Lukuki wa Zimbabwe walijaa Dimbani kuishangilia Mauritius na walilipuka kwa furaha baada ya mtanange kwisha kwa nchi yao kufuzu hatua ya Robo fainali kwa Tofauti ya magoli.
Kundi B wanamaliza michezo yao hii leo huko Bulawayo wakati Botswana wakiikabili Sheli Sheli huku Wakomoro wataumana na Waswazi.
Comoro na Botswana wanaongoza kundi wakiwa na pointi 4 kila moja , Swaziland ni wa 3 huku Sheli Sheli wametolewa kwa kuzabwa michezo miwili.
Comoro walikwenda sululu ya 0-0 na Botswana na kuzabw a 2-1 na Sheli sheli.
Waswazi wanaofundishwa na kocha wa Zamani wa Afrika ya Kusini Ephraim "Shakes" Mashaba, walianza vyema kwa kuinyoa Sheli sheli 2-1, lakini walizimwa na Botswana 1-0.
Waliojuu kisoka kusini mwa Afrika wamenyoosha moja kwa moja katika Robo Fainali ya Michuano hiyo Jumapili Wanyasa (Malawi) watakumbana na Mamba wa Msumbiji huku Namibia watawaalika wachimba Shaba wa Zambia.
Jumatatu ijayo Bafana Bafana watawaalika Angola huku Wazimba wataumana na mshindi wa Kundi B kati ya Comoro na Botswana.
No comments :
Post a Comment