Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, October 18, 2009

WACHEZAJI WA SOKA JIUNGENI SPUTANZA

Amry Massare mtangazaji wa kipindi cha Michezo na kipindi cha Viwanjani kinachorushwa siku ya Jumapili (12:00pm - 13:00pm) na mdau nambari moja wa viwanjani.blogspot.com akimuelekeza jambo katibu wa SPUTANZA Abeid Kasabalala mara baada ya mahojiano ya moja kwa moja katika kipindi cha viwanjani Radio Times FM.
Wachezaji wa soka nchini Tanzania wametakiwa kujiandikisha na kuwa wanachama katika chama cha wachezaji nchini Tanzania SPUTANZA chombo ambacho kimeundwa kupigania maslahi ya wachezaji.Hayo yamesemwa na katibu msaidizi wa SPUTANZA Abeid Kasabalala wakati akihojiwa katika kipindi cha VIWANJANI kinachorushwa na Radio Times fm Dar es Salaam kila siku ya Jumapili kuanzia saa sita kamili hadi sasa saba.
Kasabalala amesema anawashangaa wachezaji wa Tanzania hulalamika na kuhitaji msaada wakati tayari wakiwa na matatizo au mambo yanapowawia vigumu na wasijue wapi pa kukimbilia.
Amesema chombo hicho ni chao na ili waweze kukitumia wanalazimika kujiunga na kuwa wanachama.Miongoni mwa faida kubwa ambazo wachezaji wanaweza kufaidia na SPUTANZA ni pamoja na mikataba ambayo wanaingia na klabu zao lakini pia kuwasaidia kudai maslahi yao pindi wanapotimuliwa na klabu ama kusitishwa kwa mkataba wa mchezaji.
Amesema kwa sasa wameanza kutoa mafunzo maalumu kwa wachezaji ili kuwaelimisha na kuwafahamisha faida za SPUTANZA lakini pia kuwafundisha sheria mbali mbali za soka pamoja na taratibu za mikataba na wajibu wao kama wachezaji.Katibu wa chama cha wachezaji wa soka nchini Tanzania SPUTANZA Abeid Kasabalala akijibu jambo katika kipindi cha viwanjani Radio Times FM.

WASILIANA NA SPUTANZA (SOCCER PLAYERS UNION OF TANZANIA)
P.o.Box 13162, Dar es Salaam - POSTA HSE. - GHANA/OHIO AVENUE 4th FLOOR ROOM #403
SIMU - +255754270815, EMAIL: soccertanz@yahoo.com

No comments :

Post a Comment