Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Tff Rais wa Shirikisho la kandanda hapa nchini Leodga Chilla Tenga amesema Waamuzi ambao hawatachezesha mpira vizuri watawaondoa.
Aidha amewataka wachezaji kuwajibika uwanjani ili wapate nafasi ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.
Amesema ili mchezaji aweze kupata mafanikio ndani na nje ya nchi nidhamu, juhudi na kutambua wajibu wake katika klabu ndiyo jambo la muhimu.
Utovu wa nidhamu hauwezi kumfikisha mchezaji kokote zaidi kujenga chuki na mwalimu, viongozi na waamuzi uwanjani.
No comments :
Post a Comment