Timu ya taifa ya soka ya Kenya Harambee stars Jumapili itashuka dimbani kucheza na timu ya taifa ya Tunisia maarufu Carthage Eagles katika mchezo wa kusaka nafasi ya kufuzu kucheza fainali za kombe la Dunia 2010.
Kikosi hicho kitashuka uwanjani bila ya mshambuliaji wake wa kimataifa wa anayecheza soka la kulipwa nchini Ufarnsa katika klabu ya Auxxere Dennis Oliech na Macdonald Mariga.
wakati huo huo, mshambuliaji wa kimataifa wa Tunisia Lassad Nouioui amesema Carthage Eagles wamefanya maandalizi mazuri na wanaamini wataibuka na ushindi.
Kwingineko, kikosi cha Super Eagles cha Nigeria kimerejea mjini Abuja katika uwanja wa taifa kucheza na Msumbiji ikiwa ni mwezi mmoja baada ya kushindwa kuwafunga vinara wa kundi la 2 Tunisia katika uwanja huo.
Uwanja wa Abuja wenye uwezo wa kuchukua mashabiki 60,000 umetajwa pengine usiweze kujaa, kama ilivyokuwa katika mchezo dhidi ya Kenya na Tunisia.
Msumbiji wanarekodi ya kupoteza michezo miwli mfulululizo dhidi ya Tunisia na Kenya wakicheza ugenini.
Mchezo wa mwisho kushinda ni baada kuichapa Kenya 2-1 huku mfungaji akiwa Tico Tico walipocheza Maputo mwezi uliyopita na kupanda hadi nafasi ya tatu wakkiwa mbele dhidi ya wapinzani wao Kenya.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment