Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, October 10, 2009

HARAMBEE STARS KUKIPIGA NA TUNISIA

Timu ya taifa ya soka ya Kenya Harambee stars Jumapili itashuka dimbani kucheza na timu ya taifa ya Tunisia maarufu Carthage Eagles katika mchezo wa kusaka nafasi ya kufuzu kucheza fainali za kombe la Dunia 2010.
Kikosi hicho kitashuka uwanjani bila ya mshambuliaji wake wa kimataifa wa anayecheza soka la kulipwa nchini Ufarnsa katika klabu ya Auxxere Dennis Oliech na Macdonald Mariga.
wakati huo huo, mshambuliaji wa kimataifa wa Tunisia Lassad Nouioui amesema Carthage Eagles wamefanya maandalizi mazuri na wanaamini wataibuka na ushindi.
Kwingineko, kikosi cha Super Eagles cha Nigeria kimerejea mjini Abuja katika uwanja wa taifa kucheza na Msumbiji ikiwa ni mwezi mmoja baada ya kushindwa kuwafunga vinara wa kundi la 2 Tunisia katika uwanja huo.
Uwanja wa Abuja wenye uwezo wa kuchukua mashabiki 60,000 umetajwa pengine usiweze kujaa, kama ilivyokuwa katika mchezo dhidi ya Kenya na Tunisia.
Msumbiji wanarekodi ya kupoteza michezo miwli mfulululizo dhidi ya Tunisia na Kenya wakicheza ugenini.
Mchezo wa mwisho kushinda ni baada kuichapa Kenya 2-1 huku mfungaji akiwa Tico Tico walipocheza Maputo mwezi uliyopita na kupanda hadi nafasi ya tatu wakkiwa mbele dhidi ya wapinzani wao Kenya.

No comments :

Post a Comment