Na Rajabu Mhamila "Super D"
MAKAI Moringa Enterprises, jana imejitokeza kudhamini mashindano ya kumsaka malkia wa Utalii kanda ya Ilala 'Miss Utalii Ilala 2009', yatakayofanyika November 6 katika Ukumbi wa Da West Inn Park uliopo Tabata Dar es Salaam.
Udhamini wa kampuni hiyo utaigharimu sh. 750,000, ikiwa ni gharama za bidhaa zinazotengenezwa na kampuni hiyo.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Eileen Kabusi, alisema wameamua kutoa zawadi hizo za asili ili kulinda afya za warembo hao pamoja na kuvutwa kwao na mashindano hayo ya Utalii.
Mashindano hayo yatawashirikisha warembo 15, wanaoendelea na mazoezi katika ukumbi wa Dar west Park, Tabata jijini Dar es Salaam.
Warembo wengine ni Tickey Lighton (21), Agenss Deogratius(20), Grace Msuka(20), Glory Joseph(21), Violeth Mganga (21), Neema Mashala (21) na Rose Luner(21).
Wadhamini wengine katika mashindano hayo ni Chiken Hut Tanzania Limited, Savannah Lounge Paradise City Hotel, Kelken Fitness Center, Dage Saloon, Kiwanga Store & C0, Aucland Tours & Safari, The Grand Villa Hotel, Mashujaa Pub na Sayona Drinks Water.
Wengine ni Moringa Oleifera, Image Smart, Valey Spring, Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azan Zungu, VAM General Supply, Victor na Kariakoo, Mama Vanessa, Tigo, Babu Kubwa Magazine & OK News Week, Kiu, Sun, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azan.
No comments :
Post a Comment