
Akizungumza na kipindi cha michezo cha Radio Times FM Afisa uhusiano wa Kampuni hiyo Teddy Mapunda ametanabaisha kuwa mbali na kujitoa kwenye Udhamini huo lakini wanaendelea kuisaidia timu kwa kuwapa fedha ambapo wiki iliyopita waliwapa shilingi milioni 5 na wanategemea hivi karibuni kuwapa tena milioni tano.
Timu ya Toto African mpaka sasa inashika nafasi ya mwisho katika msimamo wa Ligi kuu Tanzania Bara ambapo katika michezo kumi iliyokwisha cheza imetoka sare michezo minne na kufungwa michezo yote na kujikusanyia pointi 4.
No comments :
Post a Comment