Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela amefahamisha kuwa Matayarisho yote ya mchezo huo yanakwenda vizuri na Tayari TFF imefanya vikao mbalimbali.
Amesema tiketi zinapatika katika vituo 15, vituo hivyo ni Shule ya Benjamini Mkapa,Big Bon Kariakoo, Big Bon Mbagala, Stears zote, Oil Com Veta, Uwanja wa Uhuru, Sabco Mwembe Chai, Kobil Buguruni, Njia panda ya Tabata, Sheli Ofisi ya Miundo Mbinu, Mtoni Mtongani, na vituo vyote vya plisi Tandika.
Tiketi zitaanza kuuzwa Jumatano Asubuhi katika vituo vyote ambavyo vimetajwa na tiketi hizo zitauzwa kwa siku tatu na siku ya Jumamosi hakuna tiketi itakayouzwa uwanjani siku ya mchezo wa Yanga na Simba.
Naye Katibu Mkuu wa Dar es Salaam Young Afrikan Laurence Mwalusako amesema kwamba timu yake imejiandaa vizuri katika mchezo dhidi ya Simba na amewaomba mashabiki wa Yanga wawe na nidhamu katika mchezo huo.
Akielezea kibali cha Kocha Kostadin Papic Mwalusako amesema anakifuatilia ili katika mechi ijayo awepo katika benchi
Katibu wa wekundu wa Msimbazi Simba Mwina Kaduguda alipotakiwa aelezee maandalizi ya timu yake alikuwa na haya ya kusema.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Shirikisho la Kandanda Tanzania TFF, Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu na usuluhuishi Kamanda Alfred Tibaigana amesema jana walikutana kujadili masuala hayo na walipoangalia makosa waliyoadhibiwa hayakuwa na ushahidi wa maandishi
No comments :
Post a Comment