Kwa maelekezo ya ITU  kwamba 
 huduma za televisheni za utangazaji  kubadili kutoka Analojia na kwenda
 katika   mfumo wa digitali kabla ya Juni 17, 2015, lakini kwa nchi ya 
Tanzania tarehe ya  mwisho ya kubadili mfumo ni  Desemba 31, 2012.
 Ili kuwa na uwezo wa kutekeleza 
mabadiliko haya  katika wakati, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) 
imeunda kampuni ya  Ubia na  kampuni ya Star Communication Network 
Technology Co. LTD ya  China, inayojulikana kama Star Media (Tanzania) 
LTD inayotumia jina la kibiashara la  STARTIMES. wajibu wa Kampuni hii 
ya Ubia na  ya kisasa, ni kuleta mapinduzi katika huduma za televisheni 
na utangazaji kwa njia  ya digitali na kutoa huduma za multiplex katika 
Tanzania. STARTIMES tayari imeshabadili na kuingiza katika mifumo ya 
digitali  mikoa saba  katika Tanzania Bara yaani Mwanza, Mbeya, Dodoma, 
Arusha, Moshi, Tanga na Dar es salaam. Kufikia  mwisho wa mwaka 
huu,kabla ya kubadili rasmi mfumo  mkoa wa Morogoro pia utaunganishwa 
katika mfumo wa digitali kama miko tajwa. 
Inatarajia  pia  kujenga Kituo 
cha  kurushia cha kisasa katika eneo la Makongo kilimani ili kuboresha 
signal/urushwaji wa matangazo yetu  katika Mkoa wa  Dar es Salaam  na 
baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Pwani.
Kampuni ya Star Time vile vile 
inakusudia kubadili Zanzibar na tayari tumepata  leseni kwa ajili ya 
kujenga kituo cha televisheni na kupeleka huduma za mfumo wa digitali 
kabla ya tarehe ya kubadili (Switch –off) kama kila kitu kitakwenda 
kulingana na mipango yetu. Hata hivyo, mpango wetu ni kwamba Tanzania 
nzima lazima kubadilishwa kwenda kwenye mfumo wa digitali  mapema 
iwezekanavyo ili kila Mtanzania anaweza kufurahi ulimwengu wa digitali.

No comments :
Post a Comment