Mkurugenzi wa wateja wakubwa wa kampuni ya simu za mkononi ya Zantel Ahmed Seif 
Mohamed (kushoto ) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Sh.6,040,000 kwa 
Mwenyekiti wa chama cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini (Taswa) Juma 
Pinto, pembeni ya Mohamed ni Meneja Mwandamizi wa Mawasiliano na Masoko wa 
Zantel Awaichi Mawala na Katibu Msaidizi wa Taswa, George John.
*****************************
KAMPUNI ya simu za 
mkononi ya Zantel imejitokeza kudhamini Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha 
Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) utakaofanyika Desemba 21 na 22 
mwaka huu Kiromo View Resort Hotel, Bagamoyo mkoani 
Pwani.
Akizungumza na 
waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Zantel 
Ahmed Seif Mohamed, alisema wanajisikia furaha kushirikiana na TASWA kudhamini 
mkutano huo wa aina yake.
Alisema Zantel 
imekuwa na uhusiano mzuri na wanahabari, hivyo walipoombwa hawakusita kufanya 
hivyo na wana matumaini makubwa utakuwa mkutano wenye manufaa.
Alieleza kuwa 
kampuni yake baada ya kupata mafanikio katika mashindano ya Epiq Bongo Star 
Search iliyomalizika hivi karibuni ni nafasi nyingine ya kuendelea kudhamini 
matukio mbalimbali ya michezo na burudani kwa kadri uwezo 
utakavyoruhusu.
Kwa upande 
wake Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto aliishukuru Zantel na kusema awali chama 
hicho kiliomba udhamini kwa kampuni hiyo kwa lengo la kufanya mkutano Dar es 
Salaam, lakini sasa walifikiria ufanyike Bagamoyo, Pwani.
Alisema Zantel 
wamedhamini kwa kiasi cha Sh 6,040,000 na kwamba bajeti ya mkutano huo ni Sh 
milioni 20, hivyo kuomba wadau wengine wasaidie ili kufanikisha mkutano huo 
utakaohusisha zaidi ya waandishi wa habari za michezo 100 ambao ni wanachama wa 
TASWA.
 “Mkutano huo 
unatarajiwa kushirikisha wanachama 100, na pia watakuwepo wadau mbalimbali wa 
TASWA wakiwemo waandishi wakongwe wa habari za michezo wambao watapewa nafasi ya 
kuzungumza kwenye mkutano huo,” alisema Pinto.
Kwa upande 
wake Katibu Mkuu wa chama hicho,Amir Mhando aliwasisitiza wanachama kuendelea 
kuthibitisha ushiriki wao na kuwa mwisho wa kufanya hivyo ni kesho 
alasiri.
No comments :
Post a Comment