Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, December 26, 2012

ASIA IDAROUS,GYMKHANA HILALL NA MARTIN KADINDA WATEULIWA NA KUTOA UAMUZI UNIQUE MODEL 2012



Baraza la sanaa la aifa limeteuwa majina matatu kati ya sita ya majaji  yaliopendekezwa na  waandaji wa shindano la kumsaka mwanamitindo wa mwaka mwenye sifa za kipekee.
Uteuzi huo wa wabunfu Asia  Idarous khamsini,Gymkhana Hilall (paka wear) na Martin Kadinda umefanyika mwishoni mwa wiki  hii baada ya baraza la sanaa la Taifa (Basata) kupitia wasifu wao na kuridhika wawe waamuzi rasmi wa shindano la Unique model 2012.
Kinyang’anyiro cha kumsaka mwanamitindo huyo wa mwaka kinajumuisha washiriki kumi na mbili katika jukwaa moja ambapo fainali hizi zitafanyika tarehe 28 desemba katika ukumbi wa maraha New Maisha club ulioko Oysterbay jijini  Dar.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mratibu wa shindano hilo Methuselah Magese amesema kuwa maandalizi ya shindano hilo yako vizuri sana na washiriki wamenorewa kiasi cha kutosha imebaki ni kazi ya umatiwa wapenzi wa mambo ya mitindo kujitokeza kwa wingi kushuhudia nani atachukua taji siku ya ijumaa.
Shindano la unique model litapambwa na burudani toka bendi ya mashujaa ikiongozwa na rapa maarufu Chalz Baba ikiambatana na ngoma za asili toka kwa Costa Siboka na utambulisho wa msanii mkali wa bongo flava B-shop kwa mara kwanza atatoa burudani ambayo haijawahi kutokea.
Magese aliongeza kuwa mbali ya burudani kutakuwa na zulia jekundu(Red carpet) kwa watu maarufu na watu waliopendeza zaidi siku hiyo ambapo kiingilio kitakuwa ni Tshs 15,000 tu kiingilio ambacho hakitengi tabaka la watu flani katika jamii.

No comments :

Post a Comment