Wapendwa ndugu, jamaa na marafiki 
popote pale mlipo,yamebaki masaa kadhaa kuuaga mwaka 2012, ambao kwa 
hakika ulikuwa na changamoto nyingi za kimaisha, dhoruba za hapa na pale
 wengi zilitukumba, lakini kwa kudra za Mwenyezi Mungu akatushika mkono 
akatuinua na maisha yakaendelea.
Binafsi mpaka dakika hii namshukuru 
Mungu nikiwa mwenye afya njema kabisa. Maisha ya sasa Wanadamu wengi 
wamekuwa dhaifu kwa mambo mengi, lakini Mungu ndiyo njia sahihi wa 
kumtumia katika sala zako kuyashinda majaribu na madhaifu ya Dunia. Yako
 mengi ambayo naweza nikayaandika hapa lakini bado yasitoshe pia. Nasema
 asanteni kwa ushirikiano wenu mkubwa kwa namna moja ama nyingine, kama 
kuna mahali nilikosea, tukakwaruzana kidogo basi "NAFSI NI NYONGE" 
Tusameheane na maisha yaendelee.
Tunahamia mwaka mwingine mpya kabisa 
2013, basi na tuendelee na ushirikiano huu tuliokuwa nao kwa mambo 
mbalimbali yenye kujenga na kuleta tija katika maisha yetu, Mwaka 2013 
uwe wa kuhakikisha kweli sote pia tumehamia kwenye mfumo wa kidijitali, 
tushauriane, tuelemishane tunyooshane njia iliyo sahihi ili kila mmoja 
kila wakati abaki nafsini mwake mwenye furaha daima, Pia tumtangulize 
Mungu kila wakati kwa kila jambo ili pia azidi kuzibariki kazi za mikono
 yetu daima.
Kwa Blogaz wenzangu, changamoto 
nyingi tumekumbana nazo 2012, ikiwemo tatizo kuu la KUKOPY NA KUPASTE.! 
Na nyinginezo nyingi tuzijuazo zinatusumbua kwa namna moja ama nyingine,
 basi ni nyema 2013 iwe ya kuzitafutia ufumbuzi, kama si kuzimaliza 
kabisa basi angalau tuendelee kuzipunguza ili kuzimaliza kabisa, huku 
suala la kujituma na ubunifu vikiwa ndio ngao kuu ya mabadiliko miongoni
 mwetu. Ushirikiano tuliokuwa nao umeonesha tuna uwezo mkubwa wa 
kuisadia jamii inayotuzunguka na hata serikali pia kwa namna moja ama 
nyingi, basi tusimame kidete kuhakikisha ushirikiano huu hauteteleki ama
 haupotei kirahisi, badala yake tuiimarishe zaidi kila kona.
Natoa shukurani za dhati kabisa kwa 
makampuni na wadau mbalimbali ambayo/ambao kiukweli yametoa mchango 
mkubwa kuhakikisha tunasonga mbele na libeneke hili , si vibaya 
nikiyataja makampuni hayo kuwa ni Serengeti Breweries Ltd, Airtel, 
Bayport, Msama Promotions Ltd, kampuni ya R&R, Dada Teddy Mapunda, 
Hoyce Temu, Blogaz wote (bila kinyongo) na wengine waliotupa hatua ya 
kusogea kwa namna moja ama nyingine, Mungu awabariki sana.
Asanteni 
Nawatakia heri ya sikukuu ya Mwaka mpya.

No comments :
Post a Comment