Ridhiwani Kikwete.
![]()  | 
| Assah Mwambene | 
MAANDALIZI
 ya Mkutano Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania 
(TASWA) yanaenda vizuri na wajumbe wanatarajiwa kufika Bagamoyo Ijumaa 
Desemba 28, 2012 mchana kwenye hoteli ya Kiromo View Resort watakapolala
 na kufanyia mkutano.
Ijumaa
 hiyo washiriki watatembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria Bagamoyo na
 jioni kutakuwa na mechi ya kirafiki kati ya timu ya soka ya TASWA FC na
 Bagamoyo Veterani itakayofanyika Uwanja wa Mwanakalenge na usiku 
wajumbe watakuwa na chakula cha pamoja na kubadilishana mawazo kuhusiana
 na masuala mbalimbali yahusiyo michezo na taaluma ya habari.
Mkutano
 Mkuu utafunguliwa Jumamosi Desemba 29, saa tatu asubuhi na mgeni rasmi 
atakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kusaidia timu za Taifa za Vijana, 
Ridhiwani Kikwete.TASWA imechukua jukumu la kumualika kutokana na kuwa 
mdau mkubwa na rafiki wa chama chetu.
Mkutano
 utafungwa jioni ya siku hiyo na Mkurugenzi wa Idara ya Habari 
(MAELEZO), Assah Mwambene ambaye hiyo pia itakuwa nafasi nzuri kwake 
kuweza kuzungumza na wana habari kuhusiana na masuala mbalimbali ya 
kitaaluma.
 Katika
 mkutano huo wanachama wa TASWA watapata fursa ya kupokea na kujadili 
Ripoti ya Utendaji ya chama, Mapato na Matumizi, maendeleo ya chama na 
masuala mbalimbali yanayohusu waandishi wa habari za michezo na 
maendeleo ya michezo kwa ujumla Pia
 kutakuwa na semina maalum itakayoendeshwa kwa washiriki wa mkutano huo,
 ili wawe na uelewa kuhusiana na ajenda ya kuinua kipato kwa wanachama 
ambayo nayo itajadiliwa kwenye mkutano huo.
 Kamati
 ya Utendaji ya TASWA imekubaliana iwasaidie wanachama wake waweze 
kujitegemea kwa kuanzisha Chama cha Akiba na Mikopo (SACCO’S), lakini 
imeamua kwanza iwaite wataalamu wa vyama vya ushirika watoe elimu juu ya
 jambo hilo na kukishakuwa na uelewa wa kutosha suala hilo litakuwa kama
 ajenda kamili ya kuanzisha chama hicho kwenye mkutano wetu.
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA

No comments :
Post a Comment