Ofisa
 Habari wa ngazi ya kimataifa  Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa 
(UNIC) Bi Stella Vuzo akiwakaribisha waandishi wa chama cha habari za 
Mazingira Tanzania (JET) na kuwatambulisha wazungumzaji katika mkutano 
wa taarifa fupi katika kuwapa mwanga kuhusu yatokanayo na taarifa ya 
mabadiliko ya tabianchi uliofanyika Doha. Katikati ni Mtaalam wa 
Mazingira wa UNDP Bw. Amani Ngusaro na kushoto Mkurugenzi Msaidizi wa 
Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi. 
Mkutano
 huu uliowakutanisha pamoja waandishi wa habari za Mazingira Tanzania 
(JET) umeratibiwa na Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini 
(UNIC) uliofanyika jijini Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Habari Maelezo.
Mtaalam
 wa Mazingira wa UNDP Bw. Amani Ngusaro akielezea kwa ufupi jinsi Umoja 
wa Mataifa unavyoshirikiana na Serikali ya Tanzania katika kupambana na 
mabadiliko ya Tabianchi na kufafanua Mpango wa Kupunguza Uzalishaji wa 
Hewa ya Ukaa kutokana na Ukataji miti ovyo na Uharibifu wa Misitu kwa 
nchi zinazoendelea (MKUHUMI) unaotekelezwa na Umoja wa Mataifa UN-REDD.
 Mkurugenzi
 Msaidizi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi 
akizungumzia yatokanayo mkutano wa mabadiliko ya tabianchi ikiwemo swala
 la Gesi joto ambapo amesema kwa nchi kama Tanzania haichafui mazingira 
kulinganisha na nchi zinazoendelea zenye viwanda vikubwa pamoja na 
makubaliano waliyofikikia katika mkutano huo ambayo yatatolewa na Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira hivi karibuni.
Mmoja
 wa waandishi wa habari Bi. Judica Laswai kutoka TBC akieleza namna 
alivyoweza kupata nafasi ya kuhudhuria mkutano wa mabadiliko ya 
tabianchini uliofanyika Doha hivi karibuni kwa kushiriki mashindano ya 
kuaanda vipindi vya mazingira na mwishowe kushinda safari iliyodhaminiwa
 ni Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa Tanzania (UNIC) ambapo 
amewahimiza wanahabari wenzake kutumia fursa za mitandao ya kijamii.
Pichani
 Juu na chini ni baadhi ya waandishi wa habari za Mazingira (JET) 
wakiuliza maswali na kutoa maoni kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira 
Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi (hayupo pichani).
Pichani Juu na Chini ni baadhi ya waandishi wa habari wa Mazingira (JET) waliohudhuria mkutano huo.
Ofisa
 habari Ngazi ya Taifa wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC)
 Bi. Usia Nkhoma  akitoa changamoto kwa waandishi wa habari wa mazingira
 kuzipa kipaumbele habari za mazingira  na kuwataka kuweka usawa katika 
habari wanazoandika.








No comments :
Post a Comment