Mkuu
 wa Mkoa wa Tanga Bibi Chiku Galawa akimkaribisha Makamu wa Kwanza wa 
Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad katika Mkoa huo mara baada ya 
kuwasili katika uwanja wa ndege wa Tanga.
  Makamu
 wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimia na 
vikosi vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi wa Mkoa wa Tanga, mara 
baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Tanga.
 Makamu 
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimia na 
wananchi mbali mbali waliojitokeza kumpokea wakati walipowasili katika 
uwanja wa ndege wa Tanga kwa ziara ya siku mbili. 
  
Katibu
 Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad akihutubia mkutano wa hadhara 
ulioandaliwa na chama hicho katika viwanja vya Tangamano Jijini Tanga.
 
Katibu
 Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad akionyesha kadi za ADC 
zilizorejeshwa na baadhi ya wafuasi wa chama hicho na kujiunga na CUF 
katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na chama hicho katika viwanja vya
 Tangamano Jijini Tanga.Picha na Salmin Said-Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar
----
Chama
 Cha Wananchi CUF kimesema kuwa amani ya kudumu haiwezi kupatikana 
katika nchi yoyote bila ya kuwepo haki na usawa katika jamii.
Amesema
 miongoni mwa sera za msingi za chama hicho ni kuwaunganisha wananchi, 
na kwamba umoja hauwezi kupatikana kwa kuendeleza sera za kibaguzi na 
kutowatendea haki wananchi.
Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad ameeleza hayo wakati akiwahutubia wafuasi wa CUF na wakaazi wa jiji la Tanga katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tangamano jijini Tanga.
Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad ameeleza hayo wakati akiwahutubia wafuasi wa CUF na wakaazi wa jiji la Tanga katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tangamano jijini Tanga.
“Kila
 mtu ana haki sawa na mwengine kikatiba na kila mtu anastahiki 
kuheshimiwa haki zake, kwa hivyo nasema tena kuwa popote penye ubaguzi 
hapawezi kuwa na umoja”, alisisitiza Maalim Seif.
Katika
 Mkutano huo Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa 
Zanzibar amewatanabahisha Wakuu wa Mikoa na Wilaya kufanya kazi ya 
kuwatumikia wananchi kwa uadilifu, na kuacha kushabikia masuala ya 
kisiasa.
“Kikatiba
 viongozi hawa si wanasiasa bali ni watumishi wa umma, lakini cha 
kushangaza bado wapo Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanajifanya wakereketwa wa
 vyama fulani na kuwabagua wananchi”, alieleza Katibu Mkuu huyo wa CUF.
Amewapongeza
 viongozi wa Mkoa wa Tanga kwa kuweka kando tofauti za kisiasa na 
kushirikiana na wananchi katika kusogeza mbele maendeleo ya Mkoa huo.
Mapema
 Mkuu wa Wilaya ya Tanga bibi Halima Dendegu ambaye alipanda jukwaani 
kuwasalimia wananchi waliohudhuria mkutano huo, amesema uongozi wa Mkoa 
huo unashirikiana vizuri na wananchi na wanaishi kwa kupendana na 
kuheshimiana.
Akizungumzia
 kuhusu uchumi, Katibu Mkuu wa CUF amesema chama hicho kina sera imara 
za kujenga uchumi wa Tanzania kwa lengo la kuwakomboa Watanzania 
kuondokana na hali ngumu ya maisha.
Amesema
 Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi ambazo bado hazijatumika
 ipasavyo kuweza kuwanufaisha watanzania, na hivyo kuendelea kubakia 
kuwa nchi maskini.
“Ardhi
 ya Tanzania ina rutba nzuri ambayo takriban inakubali kila aina ya 
mazao, tuna bahari ambayo nayo ina rasilimali kadhaa wa kadhaa, madini 
ya kila aina, Tanga kuna bandari na kadhalika, lakini wapi bado 
rasilimali hizi zinatumika kuwanufaisha watu wachache na makampuni ya 
kigeni na sisi Watanzani wengi tulio maskini tunabakia kushuhudia 
mashimo tu”, alifahamisha Katibu Mkuu wa CUF.
Amesema
 iwapo chama hicho kitapewa ridhaa ya kuongoza nchi mwaka 2015, 
kitahakikisha kuwa wananchi wananufaika moja kwa moja na rasilimali za 
nchi, na kwamba robo ya mapato yatokanayo na rasilimali hizo yatatumika 
kulipa madeni ya nje ambayo yameripotiwa kufikia shilingi trilioni 
ishirini (20).
Akizungumzia
 kuhusu maendeleo ya chama hicho, Maalim Seif amesema chama bado kiko 
imara na wala hakitoyumba kutokana na kujengwa na misingi ya imara.
“Watakaojaribu
 kukibomoa watashindwa, CUF hakiwezi kusambaratika hata siku moja kwa 
kuwa kimejengwa kwa misingi imara na viongozi wake wako imara na 
madhubuti kabisa”. Alifahamisha.
Katika
 risala yao wafuasi wa CUF Mkoa wa Tanga wameeleza kuwa changamoto kubwa
 inayowakabili kwa sasa ni upungufu wa dawa pamoja na kuharibika mara 
kwa mara kwa X-ray katika hospitali ya rufaa ya Bombo Mkoani humo.
Nae
 Naibu Mkurugenzi wa haki za binadamu na mawasiliano ya umma wa CUF bw. 
Abdul Kambaya amesema rasilimali zilizopo Tanzania zinatosha kuwakomboa 
wananchi na umaskini, lakini mfumo wa uongozi uliopo bado haujazingatia 
maslahi ya umma na unalenga kuwanufaisha watu wachache.
“Bandari
 ya Tanga haifanyi kazi vizuri, reli ya Tanga imekufa, mashamba ya 
mkonge yamekufa, tujiulize watu wa Tanga kuna nini?” alihoji Kambaya na 
kudai kuwa limetokana na mfumo uliopo wa uongozi. 
Katika
 Mkutano huo Chama hicho kimepoa kadi ishirini (20) za wafuasi wa Chama 
Cha ADC walioamua kujiengua katika chama hicho na kujiunga na CUF.
No comments :
Post a Comment