Serikali
 ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema matangazo ya mfumo wa Analogia 
yatazimwa rasmi katika Mikoa yote ya Zanzibar ifikapo Februari 28 
mwakani ili kupisha mfumo mpya wa matangazo kwa njia ya Dijitali.
 Waziri
 wa habari, utamaduni, utalii, na Michezo Said Ali Mbarouk ameyasema 
hayo alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari katika ukumbi wa 
Habari maelezo kikwajuni mjini Zanzibar kuhusiana na matayarisho ya 
kuhamia katika mfumo mpya wa matangazo ya Dijitali.
 
 Amesema Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Kamisheni ya 
Utangazaji Zanzibar (ZBC) zimeshauriana na kukubaliana kuwa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania iingie katika mfumo mpya wa Dijitali kwa awamu 
ambapo kwa zoni ya Zanzíbar imekubaliwa kuwa February 28 2013 ndio iwe 
mwisho rasmi wa matangazo ya Analogi.
 Waziri
 Mbarouk amesema Wizara yake haitozima mitambo ya matangazo ya Analogi 
ifikapo Disemba 31 bali itakachofanya ni kutangaza kwa pamoja matangazo 
ya Analogi na Digitali kwa mfumo unaojulikana kitaalamu kama SIMU L CAST
 hadi itakapofika muda rasmi wa kuhama mfumo wa Analogy.
 Akizungumzia
 matayarisho ambayo yamefanywa na Wizara yake katika kuukabili mfumo 
mpya wa Matangazo ya Dijitali Waziri Mbarouk amesema tayari wamejenga 
kituo cha usambazaji ishara(signals) katika eneo la Rahaleo 
kitakachokuwa na kazi ya kupokea na kusambaza ishara na mitambo ya 
uendeshaji.

No comments :
Post a Comment