Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, March 15, 2012

Bondia
wa UKRAINE VITALI Klitschko kujikita kwenye siasa

KIEV,
Ukraine
BINGWA wa uzani wa juu
unaotambuliwa na Chama cha Ngumi za Kulipwa Duniani (WBC), Vitali Klitschko
amesema hana mpango wa kuwa bondia mwenye umri mkubwa kushikilia ubingwa huo na
badala yake, amepanga kujikita kwenye ulingo wa siasa nchini Ukraine.
Shirika
la Habri la Marekani (AP), lilimnukuu bondia huyo juzi alipohojiwa kwamba
ataendelea kuzichapa kwa muda gani.
Akijibu swali hilo, bondia huyo mwenye
umri wa miaka 40 alisema haitakuwa muda mrefu na badala yake, atajikita kwenye
siasa kutokana na kwamba nchini Ukraine kuna nafasi nyingi.
Mwaka 1994 bondia
George Foreman, ndiye aliyeweka rekodi ya kuwa bondia wa kwanza kutwaa ubingwa
huo, akiwa na umri mkubwa wa miaka 45 na Klitschko, alisema kwa ujumla hataki
kuvunja rekodi hiyo ya Foreman.
Kwa sasa Klitschko ndiye kiongozi wa chama
cha upinzani kiitwacho 'Udar' (mgomo) na anataka kuwa meya wa mji wa Kiev nafasi
ambayo aliikosa mwaka 2006, wakati alipowania kwa kauli mbiu ya kupiga vita
rushwa ambapo amepania kuwa tena katika uchaguzi ambao utafanyika baadaye mwaka
huu

No comments :

Post a Comment