Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, March 9, 2012

WAZIRI MALIMA AIBIWA HOTELINI MOROGORO

Adam Kighoma
Malima

Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Adamu Kighoma Malima amekombwa vitu vyake vyote vyenye thamani ya zaidi ya sh.
milioni 15 katika hoteli ya kitalii ya Nashera ya mjini Morogoro.



Taarifa za kipolisi
zilizopatikana kutoka mjini Morogoro zimethibitisha kutokea wizi huo zikisema
ulitokea usiku wa kuamkia leo.



Zilimkariri Mkuu wa Upelelezi wa
Makosa ya Jinai mkoa wa Morogoro, Hamis Seleman taarifa zilmesema wizi umetokea
wakati waziri huyo alipokuwa amejipumzisha kwenye sebule ya chumba chake kwenye
hoteli hiyo hadi mida ya 10.45 ndipo alibaini kuibiwa vitu hivyo baada ya kurudi
chumbani.



Kwa mujibu wa polisi zimeibwa
fedha taslimu Dola 4000 za Marekani na Sh. milioni 1.5, pete mbili za silva
zenye thamani ya sh. milioni 2, simu zenye thamani ya sh. milioni 1.3,
balaghashia yenye thamani ya sh. 50,000, laptop mbili zenye thamani ya sh.
milioni 5.6, taperecorder na headphone vyote vya sh. milioni moja.



Polisi wanasema dirisha la
aluminium la chumba cha hoteli alimokuwa Malima limekutwa limevunjwa kwa kitu
kigumu.



Habari zinasema nje ya dirisha
hilo zimeoneka nyayo nje na ndani ya chumba jambo linaloashiria kuwa ni za
mwizi.



Kufuatia wizi huo, walinzi watatu
wa hotel hiyo wanashikiliwa na polisi huku taarufa zilizopatikana baadaye
tukiandaa kurusha ripoti hii zikisema kwamba baadhi ya vitu vilivyoibwa
vimepatikana, ingawa havikutajwa.

No comments :

Post a Comment