Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, July 20, 2012

CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI ZA MICHEZO TZ (TASWA) CHATUMA SALAM ZA RAMBIRAMBI AJALI YA MELI YA SKAGIT



Amir Mhando Katibu Mkuu TASWA
20/07/2012


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

(A)       AJALI YA MELI ZANZIBAR

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kinatoa pole kwa Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla kutokana na vifo vilivyotokea vya watu zaidi 60 baada ya kuzama kwa meli ya Mv Skagit juzi eneo la kisiwa cha Chumbe,Zanzibar.

TASWA inaungana na Watanzania katika kipindi hiki kigumu, huku tukiwaombea waliofariki Mwenyezi Mungu ahifadhi roho zao mahali pema na wale majeruhi awape nguvu wapone haraka waweze kuendelea na shughuli zao za ujenzi wa Taifa.

Tunaziomba familia zilizopoteza ndugu zao ziwe na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu na waamini kwamba huo ni msiba wetu sote na si wao peke yao.

TASWA inaamini wapo wanamichezo waliopoteza maisha kwenye meli hiyo na pia wapo wanamichezo waliopoteza ndugu na jamaa zao, wote tunawapa pole na wawe na moyo wa subira.

(B)         MKUTANO MKUU WA MWAKA
Kamati ya Utendaji ya TASWA inatarajia kukutana hivi karibuni pamoja na mambo mengine kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya chama hicho ikiwemo kupanga tarehe ya Mkutano Mkuu wa mwaka.

Awali sekretarieti ya TASWA ilipendekeza mkutano huo uwe mwanzoni mwa Agosti, lakini ili kuepuka kuingiliana na mwezi mtukufu wa Ramadhan mkutano huo sasa utafanyika mwishoni mwa Agosti katika tarehe na ukumbi ambao utapangwa na Kamati ya Utendaji.
 Nawasilisha.
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
20/07/2012

No comments :

Post a Comment