Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, July 21, 2012

MAISHA PLUS MSIMU WA TATU KUJA KIVINGINE




Mkurugenzi wa DMB, Masoud Kipanya akiwa katika pozi.
 
Na Mwandishi Wetu
 
SHINDANO maalum lililotamba miaka nyuma la Maisha Plus, ambalo washiriki wake hukaa kwa miezi miwili kijijini, linatarajiwa kuanza hivi karibuni kwa kushirikiana na shirika la Oxfam Tanzania, kupitia program yake ya ‘Mama shujaa wa chakula’.
 
Akizungumza kwa jana, Kiongozi Mtendaji wa kampuni ya DMB, Masoud Ali ‘Masoud Kipanya’ alisema kuwa, shindano hilo la aina yake linakuja tena kwa msimu wa tatu, likiwa na utofauti kabisa, huku mambo mbalimbali yakiboreshwa, ikiwemo mshindi kuibuka na kitita cha sh milioni 20.
 
Kipanya alisema kuwa, kwa kushirikiana na wadhamini wakuu, Oxfam Tanzania, kupitia program yao ya ‘Mama shujaa wa chakula’, ambako watapata fursa ya kuwaweka wanawake kwenye shindano, kwa kukaa ndani ya jumba hilo la Maisha Plus huko kijijini kwa wiki mbili.
 
“Kwa kushirikiana na Oxfam, shindano hili tumeborsha na litakuwa la aina yake, ambapo washiriki watakaobahatika kushiriki, watafurahia na watajifunza mengi na safari hii Mama shujaa wa chakula nao watabahatika kukaa kwa wiki mbili, kisha watatoka na washiriki wa Maisha Plus kuendelea na kinyang’anyiro cha kuwania kitita hicho cha milioni 20,” alisema Kipanya.
 
Aidha, aliwataka vijana wa kitanzania, kuchangamkia fursa hiyo, ambako wanatarajia kuanza kufanya usaili mkoani Arusha, Agosti 3 na kisha kuendelea kwenye mikoa mingine 14, ikiwemo ya Bara na viswani Zanzibar.
 
Pia, alitoa wito kwa wadhamini wengine, kutumia nafasi hii kujitokeza ili kupata kutangaza, kwani shindano hilo licha ya kufanyika misimu miwili ya 2009 na 2010, huku 2011 likishindwa kufanyika kutokana na kukosa udhamini, limejizolea sifa na kupendwa na watu wa rika mbalimbali.

No comments :

Post a Comment