Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, July 2, 2012

MAONESHO YA SABASABA




Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Dkt. Alberic Kacou akiwasili katika banda la Mfuko wa Fursa Sawa kwa wote (EOTF) wakati wa maonyesho ya 36 ya Kimataifa ya Dar es salaam yanayoendelea.Kushoto ni Afisa Mawasaliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu.
Mwenyekiti wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) Mama Anna Mkapa (kulia) akimkaribisha Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Dkt. Alberic Kacou (kushoto) katika banda la mfuko huo.


Mkurugenzi Mtendaji wa (EOTF ) Bw. Stephen Emmanuel (kulia) akisalmiana na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Dkt. Alberic Kacou. Katikati ni Mwenyekiti wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) Mama Anna Mkapa.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Dkt. Alberic Kacou akitia saini kitabu cha wageni katika banda la mfuko wa fursa sawa kwa wote (EOTF).
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Dkt. Alberic Kacou akikagua moja ya bidhaa zinazotengenezwa na wajasiriamali kutoka bara na visiwani ambao wamepewa mafunzo na mfuko huo kabla ya kushiriki maonyesho hayo. Wa pili kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa (EOTF ) Bw. Stephen Emmanuel , Mwenyekiti wa Mfuko huo Mama Anna Mkapa pamoja na Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu.
Dkt. Alberic Kacou akitazama Juisi asilia ambao haijachanganywa na kemikali yoyote zinazotengenezwa na kikundi cha Wajasiriamali wa KYM'S ENTERPRISES cha Kibaha wanaopatikana katika banda la mfuko wa Fursa Sawa kwa wote (EOSF).
Katika ziara hiyo Dkt. Alberic Kacou alikutana na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Abdallah Kigoda (Kushoto) alipotembelea banda la mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF).
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Dkt. Alberic Kacou akitazama chakula cha aina ya Senene kilichofungashwa na majani maalum ya Mgomba, Chakula hicho ni maarufu kwa wenyeji wa mkoa wa Kagera.
Afisa Mipango wa (EOTF) Bi. Rehema Batakanwa(kulia) akitoa maelezo bidhaa za Vitenge vinavyotengenezwa na Maare Enterprises kwa Dkt. Alberic Kacou (katikati) wakati wa ziara yake katika Banda la mfuko wa fursa sawa kwa wote (EOTF). Kushoto ni Mkurugenzi wa Maare Enterprises Bi. Florence Maare.
Dkt. Alberic Kacou akionekana kuvutiwa moja ya bidhaa katika banda hilo.
Meneja Mauzo na Masoko wa Moring Natural Products Christina Ngoti (kulia) akitolea maelezo ya dawa ya asili isiyonakemikali aina ya Mlonge inayotibu Mangonjwa 300 kwa Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Dkt. Alberic Kacou (katikati). Kulia ni Afisa Mipango wa (EOTF) Bi. Rehema Batakanwa.
Dkt. Ableric Kacou (kulia) akibadilishana mawazo na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dkt. Reginald Mengi pamoja na Mwenyekiti wa mfuko wa Fursa sawa kwa wote (EOTF) Mama Anna Mkapa (katikati) wakati alipotembelea banda hilo katika maonyesho ya 36 ya biashara yanayoendelea katika viwanja vya Julius Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Dkt. Alberic Kacou (katikati) akiagana na Mwenyekiti wa mfuko wa Fursa sawa kwa wote Mama Anna Mkapa baada ya kumaliza kutemebelea mabanda ya wajasiriamali waliowezeshwa na mfuko huo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa (EOTF ) Bw. Stephen Emmanuel.

No comments :

Post a Comment