Botswana imetinga hatua ya Robo fainali ya kombe la cosafa baada ya kuinyuka Shelisheli 2-0 huko Bulawayo jana usiku.
Kwa mtaji huo Botswana watakwaana na Wenyeji Zimbabwe katika hatua ya mtoano.
Botswana ipo kileleni mwa kundi B wakiwa na pointi 7 kutokana na Michezo mitatu waliyocheza mbele ya Swaziland wenyhe pointi 6 na Comoro wenye pointi 4.
Swaziland waliianza michuano ya cosafa kwa kuinyuka Sheli sheli 3-0 lakini ushindi wa jana wa Botswana umewaweka kilelelni mwa kundi lao.
Mashujaa wa Zimbabwe waliwafunga Mauritius 3-0 katika mtanange wa ufunguzi kabla ya kwenda sanjari ya 2-2 na Lesotho.
Hatua ya robo fainali ya michuano ya cosafa itaendelea tena hapo kesho wakati Wavuvi wa Ziwa Nyasa(Malawi) watapambana uso kwa Uso na Mambas wa Msumbiji huku Namibia wakijaribu kuichimba Shaba ya Zambia.
Siku ya Jumatatu Waandaaji wa Kombe la Dunia Afrika Kusini Wataulizana na waandaaji wa Mataifa ya Afrika Angola wakati ambapo watoto wa Babu Mugabe (Zimbabwe) wataumana na vijana kutoka Jangwa la Kalahari Botswana.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment