Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, October 23, 2009

BOTSWANA KUUMANA NA ZIMBABWE

Botswana imetinga hatua ya Robo fainali ya kombe la cosafa baada ya kuinyuka Shelisheli 2-0 huko Bulawayo jana usiku.
Kwa mtaji huo Botswana watakwaana na Wenyeji Zimbabwe katika hatua ya mtoano.
Botswana ipo kileleni mwa kundi B wakiwa na pointi 7 kutokana na Michezo mitatu waliyocheza mbele ya Swaziland wenyhe pointi 6 na Comoro wenye pointi 4.
Swaziland waliianza michuano ya cosafa kwa kuinyuka Sheli sheli 3-0 lakini ushindi wa jana wa Botswana umewaweka kilelelni mwa kundi lao.
Mashujaa wa Zimbabwe waliwafunga Mauritius 3-0 katika mtanange wa ufunguzi kabla ya kwenda sanjari ya 2-2 na Lesotho.
Hatua ya robo fainali ya michuano ya cosafa itaendelea tena hapo kesho wakati Wavuvi wa Ziwa Nyasa(Malawi) watapambana uso kwa Uso na Mambas wa Msumbiji huku Namibia wakijaribu kuichimba Shaba ya Zambia.
Siku ya Jumatatu Waandaaji wa Kombe la Dunia Afrika Kusini Wataulizana na waandaaji wa Mataifa ya Afrika Angola wakati ambapo watoto wa Babu Mugabe (Zimbabwe) wataumana na vijana kutoka Jangwa la Kalahari Botswana.

No comments :

Post a Comment