Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, October 17, 2009

TANZANIA YAPOROMOKA KATIKA VIWANGO VYA FIFA

Tanzania imeshuka kwa nafasi tano katika viwangi vya Fifa Dunia katika msimamo uliyotolewa mapema leo.
Tanzania ambayo katika msimamo wa mwezi uliyopita ilikuwa ikishika nafasi ya 94 hivyo imeshuka hadi nafasi ya 99.
Hata hivyo kwa Ukanda wa Afrika Tanzania imeonekana kama imepanda kwa nafasi moja kwani wakati ikishika nafasi ya 94 Duniani Afrika ilikuwa ikishika nafasi ya 23, lakini kwa sasa Afrika inashika nafasi ya 22.
Kuporomoka kwa Tanzania kumetokana na kutoshiriki katika mashindano ya mbali mbali ya kimataifa ambayo hutumiwa na shirikisho la kandanda Dunia kupandisha nchi ama kushuka katika viwango vya kandanda.
Mataifa yamepanda katika viwango vya kandanda Duniani kutokana na kucheza michezo mingi ya kusaka nafasi ya kufuzu fainali za kombe la Dunia.
Ukanda wa Afrika mwezi uliyopita Ivory Cost ilikuwa juu lakini sasa licha ya kupanda kwa nafasi ya moja lakini imeshuka hadi nafasi ya pili na nafasi ya kwanza ikishikiliwa na Cameroon ambayo imepanda kwa nafasi 15.
Wakati nambari moja Duniani inaendelea kushikiliwa na Brazili ikifuatiwa na Hispania.

No comments :

Post a Comment