Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, October 29, 2009

FIFA KUSAIDIA MPANGO WA KUKUZA SOKA TANZANIA

Raisi wa TFF Leodga Chilla Tenga(Kushoto)na Ashford Mamelod mjumbe wa FIFA.
Shirikisho la kandanda Duniani FIFA limeandaa mpango wa kukuza na kuendeleza soka kwa vijana wadogo hapa Nchini Tanzania utakaoanza mwezi March Mwakani ikiwa ni mikakati waliyonayo ya kuhakikisha mchezo huo unaendelea kukua Duniani kote.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam Mjumbe kutoka Fifa Ashford Mamelod amesema mpango huo utaanza Mashuleni kwa kuanza na vijana wakike na wakiume wa umri mdogo ambao ni muafaka kwa kuanza kufundishwa mpira.
Ashford ameongeza kuwa anahitaji ushirikiano mkubwa hasa kutoka TFF na Serikali na Wadhamini katika kuhakikisha mpango huu unafanikiwa kwa asilimia kubwa ili baadae waje kupata wachezaji wazuri wa Kimataifa.
Kwa upande wake Raisi wa Shirikisho la soka Nchini TFF Leodga Chilla Tenga amesema amefurahishwa na mpango huo ijapokuwa inahitajika nguvu za ziada katika kusimamia ikiwa ni pamoja na ushirikiano.

No comments :

Post a Comment