Ligi kuu Tanzania bara itaendelea jumapili kwa mchezo mmoja utakaopigwa uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kati ya mabingwa watetezi Yanga na Moro United.
Klabu ya Yanga imetamba kuhakikisha inaibuka na ushindi hapo kesho kufuatia kuongezewa mbinu mpya na kocha Kostadin Papic.
Afisa Habari wa Yanga Luis Sendeu amesema Yanga inakila sababu ya kuhakikisha inashinda mchezo wake wa kesho kwani wanautumia kuwa ni sehemu ya maandalizi ya kumzamisha mnyama Simba.
Yanga hadi hivi sasa imejikusanyia jumla ya pointi 15 ikishika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara.
Naye kocha wa Moro United Juma Mwambusi ametamba kuibuka na ushindi dhidi ya klabu ya Yanga kwani wanahitaji pointi zaidi ili kuchumpa kileleni mwa msimamo wa ligi.
Mwambusi amesema anauhakika wataifunga Yanga kwani msimu huu haoni kama inatisha na kuifananisha na nyanya.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment