Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, October 24, 2009

YANGA NAE KUTUPA KARATA JUMAPILI HII

Ligi kuu Tanzania bara itaendelea jumapili kwa mchezo mmoja utakaopigwa uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kati ya mabingwa watetezi Yanga na Moro United.
Klabu ya Yanga imetamba kuhakikisha inaibuka na ushindi hapo kesho kufuatia kuongezewa mbinu mpya na kocha Kostadin Papic.
Afisa Habari wa Yanga Luis Sendeu amesema Yanga inakila sababu ya kuhakikisha inashinda mchezo wake wa kesho kwani wanautumia kuwa ni sehemu ya maandalizi ya kumzamisha mnyama Simba.
Yanga hadi hivi sasa imejikusanyia jumla ya pointi 15 ikishika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara.
Naye kocha wa Moro United Juma Mwambusi ametamba kuibuka na ushindi dhidi ya klabu ya Yanga kwani wanahitaji pointi zaidi ili kuchumpa kileleni mwa msimamo wa ligi.
Mwambusi amesema anauhakika wataifunga Yanga kwani msimu huu haoni kama inatisha na kuifananisha na nyanya.

No comments :

Post a Comment