Carlos Alberto Parreira amesema kuwa anaangalia uwezekano wa kupata ofa kurudi kuwa kocha wa Afrika ya Kusini.
Mkataba wa Afrika ya Kusini na kocha wa Raia wa Brazili Joel Santana umekwisha jumatatu iliyopita na Parreira anataka kupata ofa ya kurejea tena huko Bondeni.
"kuna nafasi kama kutakuwa na ofa, itakuwa makini kwangu kuangalia hiyo amesema Perreira.
"kuna viashiria kwa Wasauzi kubaki na shule ya Brazil itakayokaa katika soka la Afrika ya Kusini ameongeza Pereira.
Parreira aliiongoza Brazil kuutwaa ubingwa wa Dunia wa Mwaka 1994 alijiuzuru kama kocha wa Afriak ya Kusini mwaka uliopita mna kwenda kumhudumia mkewe aliyekuwa mgonjwa.
Ametanabaisha kuwa kazi huko Afrika Kusini itakuwa ngumu zaidi tangu nchi hiyo kutangazwa kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia la 2010.
Bafana Bafana wamepoteza michezo michezo 8 kati ya 9 ya kimataifa iliyopita.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment