Klabu ya Simba ya Jijini Dar es Salaam imewataka wapinzani wao wa jadi Yanga kutowatupia lawama pale wanapopata tatizo na waangalie vizuri walipojikwaa na si walipoangukia.
Hayo yamesemwa na Msemaji wa Simba Cliford Ndimbo baada ya kupata taarifa kutoka Yanga kuhusu kufungiwa kwa mchezaji Moses Odhiambo na Amiri Maftah kumesababishwa na Simba.
Ndimbo amesema Ligi Kuu ya Mwaka huu imeendeshwa vizuri na makosa ambayo yanafanyika katika michezo mbali mbali inafanyiwa kazi na kutolewa maamuzi, hivyo amepongeza Shirikisho la kandanda Tanzania kwa kazi nzuri waliyoifanya katika Ligi inayoendelea.
Somba hadi sasa imejikusanyia jumla ya pointi 24 katika msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment