Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, October 7, 2009

YANGA YAZIMA NGEBE ZA TOTO - LIGI KUU TZ

Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Yanga wameendeleza wimbi la ushindi kwa timu za mikoa ya Kanda ya Ziwa baada ya kuichapa leo Toto African ya Mwanza bao 1-0 katika mchezo uliyochezwa katika uwanja wa CCM KIRUMBA jijini Mwanza.
Goli pekee la ushindi lilifungwa na mchezaji Mrisho Khalfani Ngasa katika kipindi cha kwanza baada ya kuunganisha kona iliyopigwa na Abdi Kasim.
Kufuatia ushindi huo sasa Yanga inafikisha jumla ya Pointi 14 na kushika nafasi ya pili ikiwa nyuma ya vinara wa ligi kuu ya Tanzania Bara Simba ambayo inajumla ya pointi 18.
Kwa mujibu wa Msemaji wa klabu ya Yanga Luis Sendeu amesema kikosi cha Yanga kitaondoka kesho Jijini Mwanza kuelekea Shinyanga ambapo itacheza michezo mitatu ya kirafiki katika uwanja wa Kambarage na uwanja wa Kahama, kisha itatua mkoani Singida kucheza mchezo mmoja wa kirafiki na Singida United.
Michezo mingine iliyochezwa leo katika ligi kuu Tanzania bara ni pamoja na Kagera Suger ambayo imetoka sare ya bila kufungana na Maji maji katika uwanja wa Kaitaba, Kagera.Wakati Moro United imefanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya JKT Ruvu.
Wafungaji wa Moro United ni Yona Ndabila aliyefunga goli la kwanza dakika ya 10 baada ya kuunganisha mpira wa kona uliyopigwa na Hussein Swedi, na goli la pili lilipatikana katika dakika ya 34 likifungwa na mchezaji Saidi Ahmed.
Goli la kufutia machozi la JKT Ruvu lilifungwa na Hussein Bunu katika dakika ya 45 akiunganisha krosi iliyopigwa na Sostenesi Manyasi.

No comments :

Post a Comment