Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, October 13, 2009

TWANGA PEPETA KUCHEZA NETBAL NA TASWA

Majuto Omari akipokea jezi toka kwa meneja udhamini wa Vodacom Emilian Rwejuna
Na Rajabu Mhamila Super d Mnyamwezi
TIMU ya Mpira wa miguu na Netiboli ya bendi ya muziki wa dansi ya African Star 'Twanga Pepeta' kesho itachuana na timu ya waandishi wa habari za michezo (TASWA FC) katika viwanja vya leaders, Dar es Salaam.
Mashindano hayo ni maalum kwa ajili ya kumuenzi na kumbukumbu za hayati Mwalimu Julius Nyerere ambazo hufanyika Oktoba 14 ya kila mwaka tangu aage Dunia.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa African Star Entertainment (ASET), Asha Baraka alisema, Twanga pepeta wao wapo tayari kwa kucheza na timu hiyo ambapo timu yake imejiandaa kwa ajili ya shamra shamra hizo.
Alisema, sambamba na timu za pande hizo mbili pia wasanii mbalimbali wa filamu hapa nchini watashiriki kwa pamoja katika kuadhimisha siku hiyo.
Asha alisema, baada ya bonanza hilo, wataelekea katika makazi ya Mwl. Nyerere, Msasani kwa ajili ya kufanya usafi katika makazi hayo ikiwa ni pamoja na kupanda maua katika maeneo ya makazi hayo.
Alisema,wanamuziki na wasanii wengine ikiwa pamoja na waandishi watajifunza mambo mbalimbali aliyokuwa akiyafanya Mwl. Nyerere enzi za uhai wake ikiwa ni pamoja na kufahamu makazi yake.
" Nadhani hii ni njia pekee ya kuwafanya vijana hawa kufahamu historia fupi ya Mwalimu ikiwa ni pamoja kufahamu mambo mbalimbali aliyokuwa akiyakemea na kuyapinga kama Rushwa, Udini na Ukabila ili kuepuka machafuko", alisema Asha.
Asha alisema kumbukumbu hizo zitamaliziwa na burudani ya uhakika kutoka kwa bendi hiyo linalofanyika kila siku ya jumatano katika ukumbi wa Klab Billcanas, Posta, Dar es Salaam.

No comments :

Post a Comment