Waliokuwa wadhaminui wakuu kwa miaka miwili wa timu ya Toto African ya Mwanza, ambao ni watengenezaji wa Bia ya Serengeti wamesema sababu kubwa ya kujitoa kuidhamini timu hiyo ni kutopewa ushirikiano wa kutosha na Viongozi wa klabu hiyo..
Akizungumza na kipindi cha michezo cha Radio Times FM Afisa uhusiano wa Kampuni hiyo Teddy Mapunda ametanabaisha kuwa mbali na kujitoa kwenye Udhamini huo lakini wanaendelea kuisaidia timu kwa kuwapa fedha ambapo wiki iliyopita waliwapa shilingi milioni 5 na wanategemea hivi karibuni kuwapa tena milioni tano.
Timu ya Toto African mpaka sasa inashika nafasi ya mwisho katika msimamo wa Ligi kuu Tanzania Bara ambapo katika michezo kumi iliyokwisha cheza imetoka sare michezo minne na kufungwa michezo yote na kujikusanyia pointi 4.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment