Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, October 28, 2009

MAKAI MORINGA YADHAMINI MISS UTALII ILALA

Mkurugenzi Mtendaji Makai Enterprises Eileen Kasubi ( kushoto) akiwakabidhi zawadi washiriki wa kinyang`anyiro cha Miss Utalii Ilala.

Na Rajabu Mhamila "Super D"

MAKAI Moringa Enterprises, jana imejitokeza kudhamini mashindano ya kumsaka malkia wa Utalii kanda ya Ilala 'Miss Utalii Ilala 2009', yatakayofanyika November 6 katika Ukumbi wa Da West Inn Park uliopo Tabata Dar es Salaam.
Udhamini wa kampuni hiyo utaigharimu sh. 750,000, ikiwa ni gharama za bidhaa zinazotengenezwa na kampuni hiyo.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Eileen Kabusi, alisema wameamua kutoa zawadi hizo za asili ili kulinda afya za warembo hao pamoja na kuvutwa kwao na mashindano hayo ya Utalii.
Mashindano hayo yatawashirikisha warembo 15, wanaoendelea na mazoezi katika ukumbi wa Dar west Park, Tabata jijini Dar es Salaam.Aliwataja warembo watakaopanda jukwaani ni Flora Nicholaus (22), Edna Endrew (20),Janneth Samson (19), Sheila Said Baamary (23), Sauda Ramadhani (22), Ratifa Iddy (20), Rechal Isaya(19) na Jamida Abdu (21).
Warembo wengine ni Tickey Lighton (21), Agenss Deogratius(20), Grace Msuka(20), Glory Joseph(21), Violeth Mganga (21), Neema Mashala (21) na Rose Luner(21).
Wadhamini wengine katika mashindano hayo ni Chiken Hut Tanzania Limited, Savannah Lounge Paradise City Hotel, Kelken Fitness Center, Dage Saloon, Kiwanga Store & C0, Aucland Tours & Safari, The Grand Villa Hotel, Mashujaa Pub na Sayona Drinks Water.
Wengine ni Moringa Oleifera, Image Smart, Valey Spring, Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azan Zungu, VAM General Supply, Victor na Kariakoo, Mama Vanessa, Tigo, Babu Kubwa Magazine & OK News Week, Kiu, Sun, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azan.

No comments :

Post a Comment