Wakati Tanzania ikiwa umegubikwa na mgao wa Umeme huko katika Jimbo la Kano mnchini Nigeria kimetokea kituko cha Mwaka wakati umeme ukiwa umekatika uwanjani na hivyo mchezo kuongezwa kwa dakika 14 za ziada .
Kamati ya michuano ya Jimbo hilo la Kano linalosimamia michuano ya Kombe la Dunia la chini ya miaka 17 limesema kuwa tatizo kama hilo halitotokea tena.
Matatizo hayo yalitokea katika mtanange wa kundi E baina ya USA na Hispania ikiwa nyuma kwa bao 1 Hispania ikiifunga USA mabao 2 kwa 1.
Jack McInerney aliiongozea USA kwa bao la Dakika ya 4 huku Borja akiichomolea Hispania kabla ya Pablo Sarabia kushindilia msumari wa mwisho dakika 8 baadaye.
Mtanange mwingine utaendelea kesho baina ya Malawi dhidi ya USA huku UAE wakicheza na Hispania katika kundi E.
ARGENTINA WALIZWA NA UJERUMANI
Katika Michuano ya Kombe la Dunia chini ya umri wa miaka 17 inayoendelea huku Nigeria katika Dimba la Taifa la Abuja Ujerumani imeiliza Argentina bao 1-0 goli la ushindi limesukumizwa wavuni na Mshambulizi Mario Jose katika dakika ya 8 ya mchezo.
Japan imeizima Uswisi 2-0 kwa mabao ya Mshambulizi Takumi Miyayoshi katika dakika ya 9 na 20 katika Dimba la Tesilim blogani huko Lagosi.
Usiku huu Saa tatu usiku Majira ya Afrika Mashariki Wenyewe Nigeria watawakaribisha vilivyo Honduras huko Mji Mkuu wa Abuja wakati Huko Lagos Wana Samba Brazil watachuana na Mexico.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment