Bondia Mkongwe wa ngumi za kulipwa Maneno Osward Mtambo wa gongo amewaomba waandaji wa mchezo wa ngumi kuandaa pambano dhidi yake na Bondia Mada Maugo maarufu kama Maugo Junior ili akate mdomo wa bondia huyo.
Akizungumza na kipindi cha michezo na Osward amesema Maugo bado hajui mchezo ila kazi yake ni kuongea tu na vyombo vya habari hivyo yeye ni mwalim wa kurekebisha tabia yake ya kutamba kila kukicha.
Amesema Bondia Maugo anajiona anaweza kumbe awezi na anapopigwa anadai apigwi kwa kuwa wanamaliza naye mchezo na kama atakutana naye atamsambaratisha mapema katika raundi za mwanzo za mchezo.
Hadi hii leo mabondia zaidi ya watatu wanamtaka Bondia Mada Maugo ili wamuonyeshe mchezo katika mabondia hao ni pamoja na Franciss Cheka, Karama Nyarawila na Maneno Osward.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment