Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, October 27, 2009

TIKETI ZA MCHEZO WA SIMBA NA YANGA KUANZA KUUZWA JUMATANO

Shirikisho la kandanda la Tanzania limetangaza vituo na viingilio katika Mchezo wa Dar es Salaam Young Afrikan dhidi ya watani wao wa Jadi wekundu wa msimbazi Simba mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara utakaochezwa Oktoba 31 katika Dimba la Taifa jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela amefahamisha kuwa Matayarisho yote ya mchezo huo yanakwenda vizuri na Tayari TFF imefanya vikao mbalimbali.
Amesema tiketi zinapatika katika vituo 15, vituo hivyo ni Shule ya Benjamini Mkapa,Big Bon Kariakoo, Big Bon Mbagala, Stears zote, Oil Com Veta, Uwanja wa Uhuru, Sabco Mwembe Chai, Kobil Buguruni, Njia panda ya Tabata, Sheli Ofisi ya Miundo Mbinu, Mtoni Mtongani, na vituo vyote vya plisi Tandika.
Tiketi zitaanza kuuzwa Jumatano Asubuhi katika vituo vyote ambavyo vimetajwa na tiketi hizo zitauzwa kwa siku tatu na siku ya Jumamosi hakuna tiketi itakayouzwa uwanjani siku ya mchezo wa Yanga na Simba.
Naye Katibu Mkuu wa Dar es Salaam Young Afrikan Laurence Mwalusako amesema kwamba timu yake imejiandaa vizuri katika mchezo dhidi ya Simba na amewaomba mashabiki wa Yanga wawe na nidhamu katika mchezo huo.
Akielezea kibali cha Kocha Kostadin Papic Mwalusako amesema anakifuatilia ili katika mechi ijayo awepo katika benchi
Katibu wa wekundu wa Msimbazi Simba Mwina Kaduguda alipotakiwa aelezee maandalizi ya timu yake alikuwa na haya ya kusema.Wakati huo huo wachezaji wa Dar es Salaam Young Afrikan Moses Odhiambo na Amir Maftah walioadhibiwa na kamati ya mashindano kutocheza michezo mitatu baada ya ukosefu wa nidhamu kumtukana mwamuzi katika mchezo wa Yanga dhidi ya Azam FC Oktoba 17 mwaka huu wameachiwa huru baada ya ushahidi kutokamilika.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Shirikisho la Kandanda Tanzania TFF, Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu na usuluhuishi Kamanda Alfred Tibaigana amesema jana walikutana kujadili masuala hayo na walipoangalia makosa waliyoadhibiwa hayakuwa na ushahidi wa maandishi

No comments :

Post a Comment