Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, October 29, 2009

SHIMUTA KUUNGURUMA NOVEMBA 6

Meneja wa huduma wa Mikopo Midogomidogo, Mashaga Changarawe (kushoto) akimkabidhi fulana Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Mashirika ya Umma na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMUTA) Sadiq Sagawe Dar es salaam vifaa hivyo vitakavyotumika katika mashindano ya SHIMUTA yatakayoanza mwanzoni mwa mwezi ujao anaeshuhudia katikati ni Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Award Safari.(Picha na Rajabu Mhamila)
Na Rajabu Mhamila

BENKI ya NMB imejitosa kudhamini mashindano ya Shirikisho la Mashirika ya Umma na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMUTA) yanayotarajia kuanza mwanzoni mwa mwezi ujao.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam, Meneja Mikopo Midogomidogo wa benki hiyo,Mashaga Changarawe amesema wameamua kudhamini mashindano hayo baada ya kuombwa na viongozi wa shirikisho hilo ambapo kwa kuzingatia kuwa na wao ni wanamichezo na muda mrefu ndio maana wakaamua kudhamini.''Sisi siku zote huwa tunapenda kuona nchi yetu inakuwa na maendeleo katika soka ndio maana hata haya mashirika ambayo yanashiriki mashindano hayo ndio maana tukaona si vibaya kama tukawasaidia katika kufanikisha mashindano hayo,'' alisema Changarawe.
Amesema kutokana na wao kuwa wadau wakubwa wa michezo nchini hawakuwa na budi kuwafadhili wenzao kwa namna moja ama nyingine ambapo wametoa fulana 114 zitakazotumika katika mashindano hayo.
Naye Makamu Mwenyekiti wa shirikisho hilo, Sadiq Sangawe amesema wamefurahi kupata hizo fulana, hivyo watazitumia kama inavyotakikana ambapo mashindano hayo yanatarajiwa kuanza Novemba 6 mpaka Novemba 17, mwaka huu
mgeni rasmi katika ufunguzi huo atakuwa mkuu wa Mkoa wa Tanga, Saidi Kalembo.

No comments :

Post a Comment