Meneja wa huduma wa Mikopo Midogomidogo, Mashaga Changarawe (kushoto) akimkabidhi fulana Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Mashirika ya Umma na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMUTA) Sadiq Sagawe Dar es salaam vifaa hivyo vitakavyotumika katika mashindano ya SHIMUTA yatakayoanza mwanzoni mwa mwezi ujao anaeshuhudia katikati ni Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Award Safari.(Picha na Rajabu Mhamila)
Na Rajabu Mhamila
BENKI ya NMB imejitosa kudhamini mashindano ya Shirikisho la Mashirika ya Umma na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMUTA) yanayotarajia kuanza mwanzoni mwa mwezi ujao.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam, Meneja Mikopo Midogomidogo wa benki hiyo,Mashaga Changarawe amesema wameamua kudhamini mashindano hayo baada ya kuombwa na viongozi wa shirikisho hilo ambapo kwa kuzingatia kuwa na wao ni wanamichezo na muda mrefu ndio maana wakaamua kudhamini.''Sisi siku zote huwa tunapenda kuona nchi yetu inakuwa na maendeleo katika soka ndio maana hata haya mashirika ambayo yanashiriki mashindano hayo ndio maana tukaona si vibaya kama tukawasaidia katika kufanikisha mashindano hayo,'' alisema Changarawe.
Amesema kutokana na wao kuwa wadau wakubwa wa michezo nchini hawakuwa na budi kuwafadhili wenzao kwa namna moja ama nyingine ambapo wametoa fulana 114 zitakazotumika katika mashindano hayo.
Naye Makamu Mwenyekiti wa shirikisho hilo, Sadiq Sangawe amesema wamefurahi kupata hizo fulana, hivyo watazitumia kama inavyotakikana ambapo mashindano hayo yanatarajiwa kuanza Novemba 6 mpaka Novemba 17, mwaka huu
mgeni rasmi katika ufunguzi huo atakuwa mkuu wa Mkoa wa Tanga, Saidi Kalembo.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment