Shirikisho la soka Nchini Tff limesema kwa sasa watakuwa wakali kuhakikisha Waamuzi wanachezesha mpira kwa haki kutokana la suala hilo kuzidi kukithiri katika soka nchini Tanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Tff Rais wa Shirikisho la kandanda hapa nchini Leodga Chilla Tenga amesema Waamuzi ambao hawatachezesha mpira vizuri watawaondoa.
Aidha amewataka wachezaji kuwajibika uwanjani ili wapate nafasi ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.
Amesema ili mchezaji aweze kupata mafanikio ndani na nje ya nchi nidhamu, juhudi na kutambua wajibu wake katika klabu ndiyo jambo la muhimu.
Utovu wa nidhamu hauwezi kumfikisha mchezaji kokote zaidi kujenga chuki na mwalimu, viongozi na waamuzi uwanjani.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment