Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, October 30, 2009

MWANA FA, BLACK RHINO WAANGUKA TUZO ZA CHANEL O

Wanamuziki wa Tanzania wamemwagwa katika tuzo za Video zinazotolewa na Channel O katika tamasha lililofanyika hapo jana Carnival City nchini Afrika Kusini.
Wanamuziki wa Tanzania ambao waliingia katika kinyang`anyiro cha kuwani tuzo za Video ni pamoja na MwanaFA aliyekuwa akiwaniwa tuzo ya Most Gifted East Afrca Video akichuana na Amani, Xod, Mwana Fa, Wahu, Cannibal na Black Rhino.
Black Rhino aliyekuwa akiwania tuzo mbili, moja ya Most Gifted East Afrca Video akichuana na Amani, Xod, Mwana Fa, Wahu, na Cannibal, pamoja na kuwania tuzo ya Most Gifted Hip Hop Video ambapo alikuwa akichuana na Okyeame Kwame, HHP, Zeus, Jay Ru na Pro.Wanamuziki watatu wametwaa tuzo mbili katika tuzo za Video mwaka 2009 zinazotolewa na kituo cha Televesheni cha Chennel O (2009 Channel O Music Video Awards) katika tamasha lililofanyika nchini Afrika Kusini usiku wa kuamkia leo.
Wanamuziki hao ni kutoka Nigeria, Zimbabwe na Namibia.
Darey Art Alade (Nigeria), Gal Level (Namibia) na Buffalo Souljah (Zimbabwe) ambapo kila mmoja ameondoka na tuzo mbili, na kudhihirisha umahiri wa kazi zao kwa mashabiki wa muziki barani Afrika pamoja na watazamaji wa Channel O ambao wamewachagua washindi katika sifa 14 tofauti (categoies).
Darey ametangazwa kuwa mwanamuziki bora wa kiume katika tamasha hilo lililofanyika katika ukumbi wa Carnival City Alhamisi 29 October, na kuhudhuriwa na watangazaji mashuhuri wa Afrika ambao pia walikuwa ma MC`s watatu Vuzu VJ Nonhle na Lungile na KB.
Wanamuziki ambao walitoa burudani ni 2Face Idibia, Sound Sultan, HHP (Jabba), Nneka pamoja na Bongani Fassie (Jozi) & the Umoja Choir.
Nigeria imepata tuzo tano na wanamuziki wa Afrika Kusini wamepoteza tena huku Khuli pekee akitwaa tuzo ya mwanaziki chipukizi (Best Newcomer award).

Washindi wa tuzo zote hawa hapa:

1. BEST MALE VIDEO
Darey for Not The Girl

2. BEST FEMALE VIDEO
Sasha for Only One

3. BEST NEWCOMER
Khuli for Tswak Stik'em

4. BEST DUO OR GROUP
Buffalo Souljah/Taygrin/Gal level for My Type Of Girl

5. BEST DANCE VIDEO
Lady May for Ndota

6. BEST RAGGA DANCEHALL VIDEO
Buffalo Souljah for Judgment

7. BEST AFRO POP
Gal Level for Touch Me

8. BEST KWAITO
Gazza feat. Bleksem for Passop

9. BEST R&B VIDEO
Darey for Not The Girl

10. BEST HIP HOP VIDEO
Zeus for Gijima

11. BEST AFRICAN SOUTHERN
Lizha James for Estilo Xakhale

12. BEST AFRICAN WEST
Ikechukwu for Shoobeedoo

13. BEST AFRICAN EAST
Xod for I Want You Back

14. VIDEO OF THE YEAR
Naeto C for Ki Ni Big Deal

Tuzo ya heshima imepopkelewa na - Bongani Fassie kwa niaba ya mama yake Brenda Fassie.

Tuzo za 2009 Channel O Music Video Awards itarushwa siku ya Jumapili tarehe 8 Novemba kuanzia saa 21:00, ikiambatana na bonge la show ambalo litaanza kuonyeshwa 20:30.

No comments :

Post a Comment