Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, October 10, 2009

WANJIRU YUKO TAYARI KWA CHICAGO MARATHON

Mkenya Samuel Wanjiru, ambaye alishinda katika michezo ya Olimpiki ya Beijing katika marathon mwaka jana, anatarajiwa kukutana na mpinzani mkubwa katika michuano ya Marathon itakayofanyika Chicago Jumapili hii.
Wanjiru, ambaye mwezi ujao anatimiza miaka 23, amepania kuvunja rekodi ya Dunia ya mwanariadha wa Ethiopia Haile Gebrselassie ya kukimbia saa mbili, dakika tatu na sekunde 59 mwaka jana jijini Berlin.
Lakini pia atakuwa amevunja rekodi yake ya muda mzuri wa saa 2:05.10 ambao uliuweka mwezi April jijini London.
Matokeo mazuri aliyapata katika michuano ya majira ya joto mwaka 2008 ambapo alikimbia huku hali ya hewa ikiwa ni ya joto la juu na kufanikiwa kutwaa medali ya dhahabu katika Olimpiki kwa kukimbia kwa saa 2:06.32, akiwa chini ya rekodi ya Dunia kwa dakika tatu.
Katika michuano minne aliyoshiriki ameshinda mara tatu na kushika nafasi ya pili.Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Wanjiru kuzuru nchini Marekani huku akitaraji kuchuana na wanariadha bora kumi toka Afrika, ikijumuisha wanariadha saba toka nchini Kenya, wa Morocco wawili na mmoja toka Ethiopia.
kwa upande wa Wanaume itajumuisha Abderrahim Goumri wa Morocco na Vincent Kipruto wa Kenya.

No comments :

Post a Comment