Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, October 24, 2009

LIVERPOOL v/s MANCHESTER UTD

Majogoo wa Jiji la London Liverpool wanawaalika Mashetani Wekundu Manchester United huko Anfield katika mtanange uliona gumzo kubwa katika medani ya soka Duniani.
HABARI ZA TIMU
Fernando Torres wa Liverpool ana matumaini ya kurejea Dimbani.
Glen Johnson anataraji kurejea pia lakini Injini ya Liverpool Steven Gerrard inakimbizana na muda ili kuweza kuwa kamili kutokana na majeraha.
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson amelalalma kuwa uenda akamkosa Wayne Rooney ambaye anakimbizana na Muda.
Rooney amekosa michezo miwili kutokana na kusumbuliwa na kifua, Darren Fletcher (Nyonga) yupo njiapanda huku Ryan Giggs na Patrice Evra watarejea Dimbani.
Liverpool imeifunga Manchester United nyumbani na ugenini katika msimu uliopita kwa mara ya kwanza tangu kupita miaka 7. Ushindi mkubwa ulikuwa wa 4-1 huko Old Trafford ulikuwa mzito kupewa United nyumbani kwao tangu mwaka mpya 1992.
Manchester United wameshinda mitanange 5 na suluhu 1 katika michezo 7 ya Ligi waliyocheza huko Anfield..
United wana rekodi nzuri kwa Liverpool kuliko timu yoyote ye Ligi kuu ya England wakiwa wameishinda michezo 18 na kupata pointi 61.
Liverpool
• Liverpool wamepoteza mitanange 4 muhimu katika mshindano makubwa dhidi ya Manchester United.
• Liverpool wamefunga magoli 15 kwa michezo 4 ya ligi waliyocheza Anfield kwa msimu huu.
Manchester United• katika michezo ya Ulaya na Ligi Manchester United wamechomoza mara 10 suluhu 1 katika michezo 11 waliyocheza.
• Ryan Giggs amefunga magoli 99 katika Ligi ya England huku Paul Scholes amefunga magoli 98 kwa Manchester United.
• Michael Carrick kama atateremka Dimbani atakuwa akicheza mchezo wake wa 100 wa Ligi kuu akiwa na Manchester United huku Patrice Evra na Dimitar Berbatov watakuwa wakicheza mchezo wa 100 tangu kucheza mechi za Premier League .
Fernando Torres wa Liverpool amefunga magoli 8 yote katika Ligi kuu ya England ,Kuyt amefunga magoli 4 huku mabao 3 wakiwa ni ya Ligi kuu ya England.
Kwa upande wa Manchester United Rooney ana Magoli 7 huku 6 yakiwa ni ya Ligi huku Berbatov ana magoli 3.
Katika mtanange wa hivi karibuni baaina ya Vigogo hao wawili March 14 mwaka huu Liverpool waliizaba Man Utd 4-1 magoli ya Liverpool yalifungwa na : Torres (28) Gerrard (44) kwa Tuta, Aurelio (77), Dossena (90), huku bao la kufutia machozi kwa Manchester United lilifungwa kwa njia ya Tuta na Christiano Ronaldo dakika ya 23.
Bolton Wanderer v Everton (13:30)
Hakuna majeruhi mpya katika kikosi cha Bolton ambacho kinanolewa na Gary Megson, ingawa Andy O'Brien (groin), Sean Davis (knee) na Johan Elmander (hamstring) wataendelea kukalia benchi.
Everton itamkaribisha tena uwanjani Steven Pienaar ambaye alikuwa akiuguza goti, lakini Phil Neville, Phil Jagielka, Victor Anichebe na Mikel Arteta wataendeleza kuwa nje. Leighton Baines (calf) anatiliwa mashaka, lakini Joseph Yobo atalazimika kurejea uwanjani.
Manchester City v Fulham
Robinho atakuwa tena nje kwa wiki mbili zaidi kufuatia kuumia Enka lakini Craig Bellamy atarejea. Kolo Toure anakimbizana na muda kuwa fit na Vincent Kompany atakuwapo kikosini Pablo Zabaleta yupo kolokoloni kufuatia kadi nyekundu aliyopewa wiki iliyopita.
Fulham watawakosa Danny Murphy(knee), Simon Davies (ankle), Dickson Etuhu (knee) and Andy Johnson (shoulder). Kagisho Dikgacoi anaendelea kutumikia adhabu ya kufungiwa.
West Ham United v Arsenal (16:15)
Wagonga Nyundo wa London West Ham wapo fit huku wakimkaribisha Kapteni wao Scott Parker aliyerejea kutoka korolokoloni ya soka.
Mshambulizi Eduardo anakimbizana na muda kuwa kamili Nicklas Bendtner yupo 50-50 katika kikosi cha Arsene Wenger. Theo Walcott ,Denilson na Johan Djourou wataendelea kusugua Benchi kutokana na majereha. Lukasz Fabianski na Samir Nasri watarejea uwanjani huku wakimkosa Tomas Rosicky watakapokuwa huko Upton Park.

No comments :

Post a Comment